Mbwana Samatta abadilisha Wakala
2 hours ago
Nyota wa klabu ya KRC Genk, Mbwana Samatta ameondoka katika kampuni ya uwakala ya First For Players na kujiunga na Spocs Consultant inayomsimamia Mohamed Salah wa Liverpool.
Samatta anakuwa mchezaji wa pili mwenye thamani ya juu kwa wanaosimamiwa na kampuni hiyo baada ya Mo Salah.
Samatta ambaye ni mchezaji namba mbili kwa thamani katika list ya wachezaji zaidi ya 100 wanaosimamiwa na Spocs Consultant, aliingia mkataba na First For Players December 22 2018 lakini ameamua kubadilisha wakala kwa sasa ili aweze kutimiza ndoto zake za kucheza ligi kuu ya England.